omba kwa jina langu - everyday · kwa jina langu” “na mukiomba lo lote kwa jina langu,...

32
OMBA KWA JINA LANGU Mwandishi: G. I. Harlow EVERYDAY PUBLICATIONS INC. 310 Killaly St. W. Port Colborne ON L3K 6A6 Canada Copyright © 1976 Everyday Publications Inc.

Upload: others

Post on 22-Jun-2020

5 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

OMBA KWAJINA LANGU

Mwandishi: G. I. Harlow

EVERYDAY PUBLICATIONS INC.310 Killaly St. W.

Port Colborne ON L3K 6A6Canada

Copyright © 1976 Everyday Publications Inc.

Page 2: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

ISBN 0-88873-171

Imprimé au CanadaCopyright © 1976 Everyday Publications Inc.

Page 3: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

“OMBAKWA JINA LANGU”

“Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Babaatukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwajina langu nitalifanya.” [Yoane 14:13-14]

Nani alisema maneno haya matamu katika Yoane 14:13-14?Bwana Yesu Kristo, Mwana wa Mungu. Alikuwa akifundishawanafunzi juu ya maombi, na pamoja na agizo hili kuombakwa jina lake aliwapa ahadi ya ajabu: alisema atafanya neno lolote ambalo wataomba, ili Mungu Baba atukuzwe ndani yaMwana wake.

Maombi ni nini? Ni kuomba Mungu Baba kwa jina laMwana wake, ndiye Bwana Yesu Kristo, kutupa sisi vitutunavyohitaji, na kuweka mbele yake maneno mbalimbalimengi tunayotaka afanye kwa sisi na kwa watu wengine.

Ndani ya kitabu hiki utaona kwa ufupi zaidi ya manenoambayo Neno la Mungu linatufundisha juu ya maombi. RohoMtakatifu tu anaweza kukufundisha kuomba, kama ukimpanjia kufanya hivi. Lakini sharti ujue maneno ambayo Munguanatufundisha juu ya maombi ndani ya Kitabu chake.

Kitabu hiki kina sehemu au sura 30. Utasaidiwa zaidi kamaukisoma sehemu moja kila siku ukiangalia mashairi yoteyanayotajwa ndani ya Biblia yako mwenyewe. Kwa njia hiiutaweza kujifunza maneno yote ndani ya kitabu hiki katikamuda wa mwezi mmoja.

Tunaomba Mungu aweze kutumika na kitabu hiki kidogokuongeza hamu yetu kusemezana na kushiriki na Mungu kwanjia ya maombi.

“Bwana, utufundishe sisi kuomba”(Luka 11:1)

3Copyright © 1976 Everyday Publications Inc.

Page 4: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

Maulizo juu ya MaombiWatu wanafazaika juu ya maneno mengi wakati wana-

powaza juu ya maombi. Tunataja mengine ya maneno hayahapa:

Ona mafundisho juu ya ulizo hili kwa ukurasa1. Maombi ni nini? 62. Namna gani mimi, mwenye zambi, ninaweza 7

kukaribia Mungu mtakatifu kwa maombi?3. Kwa nini inanipasa kuomba Mungu? 84. Inanipasa kuomba Mungu namna gani? 95. Inanipasa kutumia masemo ya namna gani 9

wakati ninaposema na Mungu?6. Msiyeamini anaweza kuomba Mungu? 107. Inanipasa kuomba Mungu kwa maneno gani? 118. Kuna maneno mengine ambayo Biblia inaniagiza 12

kuomba juu yao?9. Maana ya kuomba kwa “watu wote wa Mungu” 13

ni nini?10. Maana ya kuomba kwa “watu wote” ni nini? 1411. Ninaweza kuomba Bwana juu ya neno lo lote 15

kwa wakati wo wote?12. Mungu anasikia kweli wakati ninapoomba kwake? 1613,14 Mungu atajibu maombi yangu? 16,1715. Kuna neno linaloweza kuzuiza Mungu asijibu 18

maombi yangu?16. Mungu atajibu maombi yangu kila mara namna 19

ninavyotaka?

4

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Copyright © 1976 Everyday Publications Inc.

Page 5: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

ukurasa17. Maombi yangu mengi yanaweza kuchokeza 20

Mungu?18. Maana ya maombi ni kuomba tu kupewa vitu 21

tunavyotaka?19. Inanipasa kuomba mara ngapi? 2220. Inanipasa kuomba mara ngapi kwa neno fulani moja? 2221. Mara nyingine Mungu anafanya neno ninaloomba 23

kama si mapenzi yake?22. Inanipasa kwenda pahali gani kwa maombi? 2423. Inanipasa kushinda saa ngapi kwa maombi? 25 24,25 Inanipasa kukaa namna gani saa ninapoomba? 26,2726. Ni vizuri kwa mimi kuomba wakati mimi ni peke 28

yangu tu, au pamoja na watu wengine vilevile?27. Inapasa mtu kuomba namna gani kwa kusanyiko 28

la Wakristo?28. Maombi yatageuza maisha yangu kwa njia yo yote? 2929. Maombi yana faida gani kwa kazi ya Bwana? 3030. Namna gani ninaweza kujifunza kuomba? 31

Una maulizo mengine vilevile? Vizuri uyaandike juu ya karatasi.Labda utapata majibu kwa maulizo yale ndani ya kitabu hikivilevile.

5

OMBA KWA JINA LANGU

Copyright © 1976 Everyday Publications Inc.

Page 6: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~1 ~MAOMBI NI NINI?

Mtu anaomba wakati anaposemezana na Mungu juu yaneno lo lote, maneno ambayo yanamfazaisha, mahitaji yake yamwili au ya roho, maneno ambayo yanamfurahisha au kumhu-zunisha. Ni kuomba Mungu kukusaidia, kukuongoza, kukupanguvu, kuokoa wapenzi wako na ndugu zako, na manenomengi mengine usiyoweza kufanya wewe mwenyewe. Nikushukuru Mungu vilevile kwa maneno yote ambayo ana-kwisha kukufanyia. Soma Wafilipi 4:6.

Kwa mfano waza juu ya watu hawa wa Agano la Kalewalioomba kwa maneno mbalimbali:1. Yakobo aliomba Mungu kumlinda ili ndugu yake Esau

asimwumize (Mwanzo 32:9-11).2. Gideoni aliomba Bwana kumwongoza kwa njia ya ngozi

(Waamuzi 6:39).3. Hana aliomba Mungu kumpa mwana (1 Samweli 1:9-11).4. Samweli aliomba wakati aliposihi Mungu kushinda Wa-

filistini (1 Samweli 7:9-10).5. Mfalme Solomono aliomba Mungu kumpa akili ili aweze

kutawala Waisraeli vizuri (1 Wafalme 3:5-9).

6

Page 7: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 2 ~NAMNA GANI MIMI, MWENYE ZAMBI,

NINAWEZA KUKARIBIA MUNGU MTAKATIFUKWA MAOMBI?

Ndiyo, Mungu ni mtakatifu na anachukia zambi. Hawezikutazama mabaya bila kukasirika (Habakuki 1:13) na hawezikukubali wenye zambi kusimama mbele yake na zambi zaozote.

Na kweli watu wote ni wenye zambi (Waroma 3:23), nahakuna mtu hata mmoja aliye mwenye haki (Waroma 3:10).Basi NAMNA GANI watu wenye zambi wanaweza kukaribiaMungu mtakatifu? Unauliza vizuri – na utapata jibu la kuku-shangaza.

Jibu ndilo hili: kwa njia ya Kristo. Mungu alituma Mwanawake wa pekee, Mwana mpendwa, hapa duniani kufa kwawenye zambi. Kristo alibeba azabu ya Mungu kwa zambi zetuwakati alipokuwa juu ya msalaba (1 Petro 2:24), na kwa sababualijitoa mwenyewe kama sadaka kwa zambi zetu sisi tunawezakugeuka watu wa nyumba ya Mungu (Waefeso 2:19).

Kwa wakati wa sasa Bwana Yesu ni Kuhani Mkubwa wetu.Anatusimamia mbele ya Mungu na anatuombea wakati wote(Waebrania 7:25). Kwa sababu hii mwandishi wa barua kwaWaebrania anatuagiza kukaribia kiti cha neema pasipo woga, ilitupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wamahitaji (Waebrania 4:16). Hivi tunaweza kuja kupata neemakwa njia ya maombi.

7

OMBA KWA JINA LANGU

Page 8: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 3 ~KWA NINI inanipasa

kuomba Mungu?

Ninaamini ya kwamba Mungu ananipenda na ya kwambaanaongoza maneno yote ambayo yananipata. Ninaamini anajuamahitaji yangu na anatuma kwangu maneno yale tu yaliyo kwabaraka yangu. Basi kwa nini anataka mimi kuomba kwamaneno haya?

Unataka kujua kwa nini inakupasa kuomba? Ni kwasababu:

1. Mungu anataka ufanye hivi. Mungu ni kama baba yadunia anayejua mahitaji ya mtoto wake lakini anayetaka mtotokumwomba kwa vitu vile anavyotaka. Mungu anataka sisi wa-toto wake kufika mbele yake kwa maombi kwa sababu anatu-penda na anapenda kusikia sauti zetu. Anataka tumtegemeekwa mahitaji yetu yote kwa sababu anajua neno hili litatusaidiakukaa karibu naye.

2. Mungu anakuagiza kufanya hivi. Neno hili ni nenokubwa sana. Tunaagizwa kuomba siku zote, pasipo kuchoka(Luka 18:1). Soma vilevile Luka 21:36; Waefeso 6:18 na 1 Wa-tesalonika 5:17.

8

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 9: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 4 ~Inanipasa kuomba Mungu

NAMNA GANI?1. Tumesema mbele ya kwamba Mungu ni mtakatifu na

haifai tusahau neno hili kamwe wakati tunapoomba. Shartitukumbuke ya kwamba yeye ndiye Mwumba wetu nasi tuli-umbwa naye. Hivi yeye ni mkubwa kupita sisi na ingetupasakufika mbele yake na unyenyekevu na kumwonyeshea heshi-ma wakati tunaposema naye.

2. Mungu anataka sisi kuomba na roho ya kweli, si na uda-nganyifu. Haifai tuseme tu maneno fulani na kinywa nakuwaza maneno mengine rohoni (Zaburi 145:18). Ingetupasakuomba juu ya maneno yetu wenyewe wakati sisi ni peke yetupamoja na Mungu. Tukiomba juu ya maneno haya mbele yawatu wengi, labda watafikili sisi ni Wakristo wazuri sana.Haifai kuomba kwa kuonekana mbele ya watu. Soma manenoBwana Yesu aliyosema juu ya neno hili katika Matayo 6:5-6.

~ 5 ~Inanipasa kutumia

MASEMO YA NAMNA GANIwakati ninaposema na Mungu?

Vizuri tumwambie tu waziwazi maneno tunayotaka yeyekujua na maneno tunayotaka ayafanye. Haifai tutumie manenomarefu, au maneno wenye elimu wanayotumika nayo, walakuomba maombi marefu kama wapagano wanavyofanya wa-kati wanapoomba kwa miungu yao (Matayo 6:7).

Bwana Yesu alitupa sisi mfano mzuri sana wa namna ganianataka sisi kuomba. Soma Matayo 6:9-13 polepole na ona ya

9

OMBA KWA JINA LANGU

Page 10: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

kuwa ombi hili linajaa na heshima kwa Mungu na ya kwambamasemo Bwana Yesu aliyotumia si masemo ya elimu. Tutawazajuu ya mashairi haya tena nyuma.

~ 6 ~MSIYEAMINI anaweza

kuomba Mungu?Zaidi ya wasioamini hawana hamu kuomba Mungu. Lakini

mara nyingine Mungu anachokoza zamiri zao kwa njia yakutuma taabu au hatari kwao na halafu wanalia kwake awasai-die. Wabaharia katika Yona 1:14 walifanya hivi. Mara nyinginewatu namna hii wanaahidi Mungu ya kwamba watageukawafuata wake na kumtumikia kama akiwaponyesha toka taabuyao. Mungu anasikia na kujibu maombi ya namna hii? Bilashaka anayasikia na mara nyingine anayajibu vilevile.

Kuna ombi moja mtu asiyeokolewa kwanza analoweza ku-omba na bila shaka Mungu atajibu ombi hili na furaha. Ni ombiambalo mtoza kodi aliomba hekaluni (Luka 18:13). Mtu huyualijua ya kwamba alikuwa mwenye zambi na hakustahili kufi-ka karibu na Mungu. Alikuwa na huzuni juu ya zambi zake naalichoka nazo, hivi aliomba Mungu na unyenyekevu kabisakumrehemu na kumsamehe. Unafikili Mungu alijibu ombilake? Kabisa! Ona shairi 14. Anafanya vivyo hivyo kwa kilamwenye zambi anayetubu na kufika kwake na unyenyekevukwa kuomba usamehe. Ndiyo, na kuna furaha kubwa mbingu-ni juu ya kila mtu mwenye zambi anayetubu (Luka 15:7). Hilindilo ombi la kwanza inalopasa kila mtu kuomba.

10

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 11: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 7 ~Inanipasa kuomba Mungu

KWA MAMBO GANI?Soma Luka 11:2-4 tena. Haya ndiyo masemo ya Bwana Yesu

mwenyewe. Tunaagizwa kuomba 1. kwa Mungu Baba kutukuzwa. Kwa pahali pengine Bwana

Yesu alisema ya kwamba atafanya neno lo lote tunaloombakwa jina lake ili Baba Mungu atukuzwe ndani ya Mwana(Yoane 14:13).

2. mapenzi na makusudi ya Mungu yafanyike duniani.Tusaidie kutimiza maombi haya kwa njia ya kufanyamapenzi yake sisi wenyewe (Zaburi 40:8).

3. Baba kutupa sisi vyakula tunavyohitaji kila siku.Ameahidi kutupa sisi vitu vyote tunavyohitaji kama tuki-weka ufalme wake na haki yake kwanza (Matayo 6:33).

4. Baba kusamehe zambi zetu – kama vile tukiwasamehewale ambao walitukosea sisi. Bwana Yesu alituambia wazikabisa katika Matayo 6:15 ya kwamba Mungu hatasamehezambi zetu kama sisi tusiposamehe mabaya ambayo watuwengine walitutendea vilevile.Ona ya kwamba ndani ya ombi hili utukufu wa Mungu na

mapenzi yake ni kwa pahali pa kwanza, si mahitaji yetu namaneno yetu mengine.

11

OMBA KWA JINA LANGU

Page 12: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 8 ~Kuna maneno mengine ambayo Biblia

inaniagiza kuomba juu yao?Ndiyo, Biblia inatuagiza kuomba juu ya maneno mengine

vilevile. Tunaagizwa kuomba:1) kwa wale ambao wanatutesa (Matayo 5:44). Bwana Yesu

alifanya hivi yeye mwenyewe (Luka 23:34), na mtumishiwake Stefano alifanya vivyo hivyo (Matendo 7:60). Ninguvu kufanya neno hili lakini litatusaidia kushindawakati tunapoteswa kwa sababu ya imani yetu.

2) ili tusishindwe na majaribu (Matayo 26:41). Bwana aliahi-di ya kwamba hatutajaribiwa kupita kipimo chetu, lakiniwakati tunapojaribiwa atatupa sisi nguvu kuvumilia naatafanya vile njia kwa sisi kuweza kutoka ndani yamajaribu yenyewe (1 Wakorinto 10:13).

3) Bwana kutusaidia wakati tulipo na ugonjwa au taabunyingine (Yakobo 5:13). Bwana Yesu anatuhurumia katikauzaifu wetu, wa mwili, na wa roho vilevile (Waebrania4:15), naye anatuombea siku zote mbele ya Mungu(Waebrania 7:25). Ni ajabu kabisa!

4) kwa watawala walio na amri juu yetu (1 Timoteo 2:1-2).Na pamoja na kuwaombea inatupasa kuwatii (Waroma13:11) na kuwaheshimu.

5) kwa wale wanaotumikia Bwana. Paulo alisihi Wakristotena na tena kumwombea (Waroma 15:30-31; Waefeso 6:19;1 Watesalonika 5:25; 2 Watesalonika 3:1). Kila mtumishi waMungu anafahamu ya kwamba anapiga vita na adui yakeShetani na ya kwamba anahitaji sana maombi ya Wakristo.Unaweza kushiriki katika utumishi wake kwa Bwana, nazawabu yake, kwa njia ya kumwombea kila siku!

12

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 13: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

6) ili Mungu, Bwana wa mavuno, aweze kutuma watumishiwengine kukusanya mavuno yake (Matayo 9:38). Watuwengi zaidi wangeamini Bwana Yesu kama watu wengizaidi wangekuwa tayari kuwapasha habari zake. Wale tuwanaweza kuomba ombi hili na roho ya kweli walio tayarikwenda wao wenyewe kama Bwana akitaka kuwafanyawavunaji katika shamba lake.

~ 9 ~Maana ya kuomba kwa

“WATAKATIFU WOTE” ni nini?[Waefeso 6:18]

Maana yake ni wazi tu – ni kuombea Wakristo wote! 1) Ni watu wale wa jamaa yako walio katika Kristo. Unataka

walindwe katikati ya majaribu mengi ambayo yanawazu-nguka, na kukaa kufuata Bwana? Kama ni hivi, shartiuwaombee. Vizuri uombe Mungu vilevile kukupa mape-ndo na ufahamu na uvumilivu wakati unapokaa katikatiyao ili uweze kuwasaidia vizuri.

2) Ni rafiki zako Wakristo na wale unaoshiriki nao kanisanina kwa kazi ya Mungu.

3) Ni wazee wa kanisa lako. Omba Mungu kuwapa akilinyingi na nguvu kwa kazi yao ya kuongoza na kusaidiaWakristo wengine na kuongoza maneno ya kanisa.Wakristo wote wakiombeana, hakutakuwa na wivu namagomvi na mabishano katikati yao. Ni kazi ya wazeekuchunga utaratibu.

4) Ni watumishi wa Mungu wanaotumia saa zao zote kwakazi ya Bwana. Omba Mungu a) waweze kuwa wanyenyekevu na kutembea karibu sana

naye;

13

OMBA KWA JINA LANGU

Page 14: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

b) abariki kazi wanayofanya kwaye;c) aweze kuwapa vyote wanavyohitaji kwa njia ya roho,

mwili, na mali. Unaweza kuongeza matunda yao kwakazi ya Bwana kwa njia ya kuwaombea.

Kwa wakati wa sasa Bwana Yesu Kristo anatuombea sisi(Waebrania 7:25), na tuko karibu zaidi naye wakati tunapo-fanya kazi hii vilevile, ndiyo kuombea watu wake.

~ 10 ~Maana ya KUOMBA KWA

“WATU WOTE” ni nini?[1 Timoteo 2:1]

Ni kuomba kwa wasioamini ndani ya jamaa yako. Hakunamtu mwingine ambaye atawaombea isipokuwa wewe! Ni kaziyako kabisa.

Ni kuombea vilevile wasioamini wanaokaa ndani ya nyu-mba kando ya nyumba yako, na wale unaotumika kazi pamojanao au kukutana nao kwa njia mbalimbali. Omba Bwana:

1) kukupa akili wakati unapojaribu kuwapasha HabariNjema;

2) kuwasaidia kufahamu na kukubali ya kwamba wao niwenye zambi, wapotevu;

3) kuwapa hamu kugeuka Wakristo kwa sababu wana-weza kuona Kristo ndani ya maisha yako;

4) kuwapa imani na kuwasaidia kupokea Bwana YesuKristo kuwa Bwana na Mwokozi wao wenyewe.

Kuomba kwa watu wote ni kuomba kwa milioni za watukatika dunia nzima wasiojua bado Habari Njema, ili wawezekuisikia na kuokolewa.

14

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 15: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 11 ~Ninaweza kuomba Bwana juu ya

NENO LO LOTE kwa WAKATI WO WOTE?Ndiyo; na zaidi ya ile tunaagizwa kuomba kwa kila wakati

katika roho (Waefeso 6:18). Hata ukifanya maneno gani, inge-kupasa kuomba Bwana juu yao.

Unatembea ndani ya motokari? Omba Bwana kukulinda.Wewe ni kwa pahali pa kazi? Omba Bwana kukusaidia

kufanya kazi yako kwa utukufu wake.Unavua mavazi au kupika vyakula au kufanya kazi

nyingine nyumbani? Omba Bwana kukusaidia na kukupa fura-ha kwa kazi ya kuchunga bwana na watoto ambao Mungualikupa.

Una watoto? Halafu inakupasa kuomba Bwana tena na tenakukupa saburi na ufahamu wakati unapojaribu kuwafundishana kuwaongoza kutembea vizuri.

Omba Mungu wakati unapokwenda shambani au dukani,wakati unapofundisha watoto siku ya Bwana, wakati ulipomgeni nyumbani mwa watu wengine au wakati unapopokeawageni nyumbani mwako. Ndiyo, omba kwa kila wakati.

15

OMBA KWA JINA LANGU

Page 16: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 12 ~Mungu ANASIKIA kweli wakati

ninapoomba kwake?Ndiyo, Mungu anatusikia wakati tunapoomba. Mwandishi

wa Zaburi 4:3 alijua neno hili kabisa. Soma vilevile Zaburi 6:9na 34:17. Nabii Mika alijua vilevile ya kwamba Mungu ata-msikia (Mika 7:7). Yona alililia Bwana wakati alipokuwa katikataabu kubwa na Bwana alimsikia (Yona 2:2). Sharti usomemashairi haya ndani ya Biblia yako mwenyewe!

Lakini kuna neno moja litakalofunga masikio ya Munguasisikie maombi yetu. Hatusikii wakati tunapofanya zambi nahatujakiri zambi hii bado (Isaya 59:2).

~ 13 ~Mungu ATAJIBU maombi yangu?

Ndiyo, Mungu anakusikia, na zaidi ya ile ameahidi kujibumaombi yako. Soma mashairi yanayofuata polepole na kuwazasana juu yao:

“Ombeni na mutapata” (Luka 11:9).“Kama mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya”

(Yoane 14:14).“Kama mukikaa ndani yangu, na maneno yangu yanakaa

ndani yenu, mutaomba neno gani munalotaka na mutafanyizi-wa” (Yoane 15:7).

“Neno lo lote tunaloomba tunalipokea kwake kwa kuwatunashika amri zake na kutenda maneno yanayopendezamachoni mwake” (1 Yoane 3:22).

“Vitu vyote mutakavyoomba katika maombi kama muki-amini, mutapokea” (Matayo 21:22).

Tushukuru Mungu wetu kwa ahadi hizi kubwa.

16

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 17: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 14 ~

Wakati unapowaza juu ya mashairi haya utaona ya kwa-mba Mungu atajibu maombi yetu kama:1) tukiomba kwa jina la Bwana Yesu (Yoane 14:14). Maana ya

kuomba kwa jina lake ni nini? Ni kuomba kwa nenolinalopatana na mapenzi yake. Ukifanya neno kwa jina lamtu mwingine, ni kusema unafanya neno yule mtu mwi-ngine analotaka lifanywe. Hivi kuomba kwa jina la Kristo sikusema tu kwa mwisho wa maombi yako: “Ninaomba hivikwa jina la Kristo,” lakini ni kuomba kwa maneno yaleyanayopatana na mapenzi yake.

2) tukikaa ndani ya Kristo na maneno yake yakikaa ndaniyetu (Yoane 15:7). Maana yake nini? Kukaa ndani ya Kristoni kuwa na upatano wa karibu sana naye. Maneno yake ya-nakaa ndani yetu wakati tunapoyasoma kila siku nakuwaza juu yao na kuongozwa nao kwa maneno tunayo-fanya na kusema. Maneno haya ni kweli ndani ya maishayako? Halafu unataka maneno yale tu yanayopatana namapenzi ya Mungu na unaweza kujua ya kwamba Munguatajibu maombi yako wakati unapoomba kwa maneno haya.

3) tukitii maagizo yake na kumpendeza ndani ya maishayetu ya kila siku (1 Yoane 3:22). Wakristo si chini ya sheriaya Musa sasa, lakini Bwana ametupa sisi maagizo mengindani ya Agano Jipya. Hivi ni lazima kwako kujua manenoyanayoandikwa ndani ya Agano Jipya ili uweze kujua kamaBwana akitaka wewe kufanya nini. Halafu sharti utii ma-agizo haya kama ukitaka Bwana kujibu maombi yako.

4) tukiwa na imani, maana yake kama tukiamini ya kwambaBwana atatujibu (Matayo 21:22; Marko 11:24). Usifikili uta-pata kitu kutoka kwa Bwana kama ukiwa na shaka nakufikili kwamba labda hatajibu maombi yako (Yakobo 1:5-8). Usiombe namna waamini nyumbani mwa Maria wali-vyoomba wakati Petro alipokuwa gerezani. Waliomba

17

OMBA KWA JINA LANGU

Page 18: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

Mungu aweze kuondosha Petro toka gereza, lakini walise-ma kijakazi alikuwa na wazimu wakati alipowaambia yakwamba Petro alisimama kwa mlango wa nyumba!Hawakuamini kabisa kabisa ya kwamba Mungu atajibumaombi yao! Soma Matendo 12:5-17.Lakini Hana aliomba na imani kweli (ona 1 Samweli 1:1-18).

Hana alikuwa na huzuni sana kwa sababu hakuwa na mtoto naalililia Bwana akimwomba kumpa mwana. Aliamini ya kwa-mba Mungu alikuwa amesikia maombi yake na atamjibu, nakwa sababu hii hakuwa na huzuni tena (sh.18).

~ 15 ~KUNA NENO LINALOWEZA KUZUIZA

MUNGU ASIJIBU MAOMBI YANGU?Ndiyo, Biblia inaonyesha maneno machache yanayozuiza

Mungu asijibu maombi yako mara nyingine. Ni maneno haya:1. Zambi usizokiri bado. Tuliona neno hili mbele katika Isaya

59:1-2. Soma Zaburi 66:18 vilevile. Shairi hili ni shairikubwa sana. Halafu inakupasa kufanya nini? Kukiri zambiyako, ili Mungu aweze kukusamehe na kukusafisha tokauzalimu wote (1 Yoane 1:9)!

2. Udanganyifu wa moyo. Mungu hatajibu maombi yakokama ukiomba kwa kuonekana mbele ya watu kusudi watuwafikili wewe ni Mkristo mzuri sana. Ona Matayo 6:5;23:14; Marko 12:40.

3) Ukosefu wa upatano katikati ya mume na mke. Ingepasamume na mke kukaa pamoja na salama, mume akipendamke wake na kumchunga, na mke akitii mume wake. Isi-pokuwa hivi, Mungu hatajibu maombi yao (1 Petro 3:1-7).

4) Makusudi mabaya. Mara nyingine watu wanaombaMungu kwa vitu wanavyotaka kwa faida au furaha yaowenyewe, si vitu visivyo kwa utukufu wa Mungu. Munguhatajibu maombi haya (Yakobo 4:3).

18

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 19: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 16 ~Mungu atajibu maombi yangu kila mara

NAMNA MIMI NINAVYOTAKA?

Sivyo. Mara nyingine atakupa kitu kizuri kupita au ku-fanya neno lingine. Inawezekana kwa wewe na mimi kuombaMungu kwa kitu tunachofikili ni kitu kizuri, kitu kitaka-chotukuza Mungu, lakini Baba yetu anayejua maneno yote ana-jua kitu hiki kingeumiza kazi yake na kutuumiza sisi vilevile.Mungu Baba anapenda watoto wake, na hivi, kwa pahali pakutupa sisi kitu tunachoomba anatupa kitu kilicho kizuri kupi-ta, kitu kitakachokuwa baraka kwetu na kumtukuza yeye.Anajibu maombi yako – si namna wewe ulivyotaka, lakini kwanjia ya kukupa yaliyo bora kuliko yale uliyoomba!

Tunaweza kuona neno hili katika maisha ya Paulo. Pauloalikuwa na uzaifu mmoja mwilini ambao ulimtesa sana. Ali-fikili uzaifu huu ulimzuiza ndani ya kazi yake kwa Bwana, hivialiomba Bwana mara tatu kuuondosha kwake. Lakini Bwanahakufanya neno Paulo aliloomba. Kwa pahali pa kuondoshauzaifu wake Mungu alijibu hivi: alimpa Paulo neema yakutosha kubeba uzaifu na kuumia mwilini mwake na kumtu-kuza hata hivi. Halafu Paulo alianza kushukuru Mungu kwauzaifu wake kwani alijuana na neema ya Mungu kupita mbelekatika maisha yake kwa sababu ya neno hili (2 Wakorinto 12:7-9). Mara nyingi Mungu hatuondoshi katika taabu yetu wakatitunapomwomba kufanya hivi, lakini anatupa nguvu ku-mtukuza hata ndani ya taabu yenyewe. Tumshukuru katikamambo yo yote.

19

OMBA KWA JINA LANGU

Page 20: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 17 ~

MAOMBI YANGU MENGIYANAWEZA KUCHOKEZA MUNGU?

Sivyo! Yakobo anatuambia ya kwamba tunakosa vitutunavyotaka kwa sababu hatuombi Mungu kwa vitu hivi(Yakobo 4:2). Ni nguvu kwawe kuwa na saburi? UmeombaMungu kukupa saburi? Hapana? Basi huwezi kutoa uzuru juuya kukosa saburi kwani Bwana ni tayari kukupa saburi kamaukimwomba kufanya hivi.

Maneno yote yanawezekana na Mungu na hakuna nenolinaloweza kumshinda (Mwanzo 18:14; Matayo 19:26), nayeanatukuzwa wakati tunapoomba maneno makubwa kwaketukiamini ya kwamba atayafanya. Kama ukimwomba, ataku-wezesha kufanya maneno usiyoweza kamwe kufanya kwanguvu yako mwenyewe.

Waza juu ya Elia. Wakati Waisraeli walipokuwa wame-kwenda mbali na Bwana na kuabudu mungu Bali, Elia aliombaMungu kufanya neno lisilowezekana kwa watu (1 Wafalme18:17-39). Yeye na watu wote wa Israeli walikusanyika kwamlima wa Karmeli pamoja na manabii 400 wa Bali.

Basi Elia alitaka Mungu kufanya neno litakaloaminishawatu wote ya kuwa yeye ndiye Mungu wa kweli. Aliwekasadaka ya ngombe juu ya mazabahu na kumwanga mapipakumi na mawili ya maji juu yake hata kuni na sadaka juu yamazabahu zilioza kwa maji. Kisha aliomba Bwana kuonyeshaya kwamba yeye ndiye Bwana Mungu ili watu wa Israeliwaweze kurudi kwake. Mungu alijibu maombi ya Elia kwa njiaya kutuma moto kuteketeza sadaka hata kama ilioza kwa maji.Halafu watu wote walishangaa kabisa, wakaanguka kifudifudina kukiri ya kwamba Bwana ni Mungu wa pekee wa kweli.Hivi Mungu alitukuzwa kwa sababu Elia alikuwa na imani naalimwomba kufanya ajabu!

20

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 21: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 18 ~

MAANAA YA MAOMBI NI KUPEWA TU VITU TUNAVYOTAKA?

Sivyo. Sehemu kubwa ya maombi ni sifa na mashukuru.Ndani ya Wafilipi 4:6 Paulo anatufundisha ya kwamba ingetu-pasa kuomba pamoja na kushukuru Mungu kila mara. SomaWakolosayi 4:2 vilevile. Ingetupasa kushukuru Mungu sikuzote kwa mambo yote, katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo(Waefeso 5:20). Labda unafikili ni nguvu kushukuru Mungukwa maneno fulani. Ni kweli, lakini hata hivi tunaagizwakufanya hivi. Kumbuka ya kwamba Mungu anafanyiza manenoyote kuwa baraka kwetu (Waroma 8:28). Soma vilevile 1 Wa-tesalonika 5:18 na tia mstari chini yake ndani ya Biblia yako.

Waandishi wa Zaburi walikuwa na sifa na shukrani mengikwa Mungu. Ona Zaburi 26:7; 92:1; 95:1-2; 100:4. Usikose kuso-ma mashairi haya ndani ya Biblia yako.

Labda una majirani ambao walikuomba kuwasaidia ndaniya maneno fulani? Nawe ulitoa saa yako na kutumia mali yakokufanya hivi, lakini nyuma yake hawakuleta hata asante kwamasumbuko yako. Halafu ulifikili nini? Ungependa kuwasaidiatena? Siku moja Bwana Yesu alisafisha wakoma kumi. Alifikilinini wakati mmoja tu wa wakoma wale kumi aliporudi kumpaasante kwa sababu alimponyesha? Soma Luka 17:12-18. BasiMungu anafikili nini wakati tunapoomba maneno karibu nayesiku zote lakini hatumshukuru wakati anapojibu maombi yetu?

Mungu anataka sisi kuomba kwa sababu gani? Tunaonasababu moja hapa: ili tuweze kumsifu na kumshukuru wakatianapojibu maombi yetu. Tunamtukuza wakati tunapomtoleazabihu ya kushukuru (Zaburi 50:23).

Kwa sababu gani basi tutanyima Mungu mashukuru yetu?Ametupa Mwokozi wa ajabu (2 Wakorinto 9:15), na ndani yaMwokozi huyu ametubariki na baraka zote za roho. Anatulinda

21

OMBA KWA JINA LANGU

Page 22: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

(1 Petro 5:7), na ameahidi kutupa sisi vitu vyote tunavyohitajitungali hapa duniani (Matayo 6:25-33). Anaweka roho sana juuyetu (Matayo 10:29-31), na kutazamia siku wakati atakapo-tukaribisha kwake mbinguni kwa milele na milele (Yoane 14:1-2).

~ 19 ~INANIPASA KUOMBA

MARA NGAPI?Kwa nini unauliza neno hili? Unaogopa ya kwamba Mungu

atachoka na maombi yako?Ni kweli ya kwamba zaidi ya watu wanachoka mbio wakati

tunapoomba vitu karibu nao tena na tena, lakini Mungu ninamna nyingine na watu. Anafurahi sana kwa watoto wakekufika kwake na maombi kwa kila wakati. Nabii Danieli ali-omba Bwana mara tatu kila siku (Danieli 6:10). Daudi alifanyavivyo hivyo (Zaburi 55:17).

Bwana Yesu alisema ya kwamba ingepasa watu kuombasiku zote (Luka 18:1). Katika 1 Watesalonika 5:17 tunaagizwakuomba pasipo kuacha. Ni kusema ya kwamba kwa saa yo yotemchana au usiku unaweza na inakupasa kuomba Mungu kwamahitaji yako mwenyewe na kwa mahitaji ya watu wenginevilevile.

~ 20 ~INANIPASA KUOMBA MARA NGAPI KWA

NENO FULANI MOJA?

Maandiko Matakatifu hayatupashi jibu la ulizo hili, lakinitunaagizwa kudumu katika maombi (Wakolosayi 4:2). Mtummoja wa jamaa yako hajaamini Kristo bado? Halafu ombeamtu huyu kila siku kufika wakati anapopokea Kristo kuwaMwokozi wake. Labda itakupasa kuomba miaka mitano aukumi au zaidi.

22

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 23: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

Kuna neno fulani unalotaka sana na umeomba Mungu juuyake, lakini ni kama Mungu hakujibu? Kaa kuomba tu juu yaneno hili, lakini bila kusema na Mungu ya kwamba ni lazimakwake kujibu maombi yako na kufanya neno unaloombakwake. Inakupasa kuomba namna Bwana Yesu alivyoombakatika shamba la Getesemane, “Si kama ninavyotaka mimi,lakini kama wewe unavyotaka” (Matayo 26:39). Labda nenounaloomba halipatani na mapenzi ya Mungu hata kama weweukifikili lingekuwa vizuri. Kwa mfano, labda una rafiki mmojaaliyetumikia Bwana sana sana kufika wakati aliposhikwa naugonjwa. Sasa analala kitandani kwa majuma mengi naumeomba Bwana kumponyesha ili aweze kumtumikia tena.Lakini Mungu hamponyeshi. Kwa nini? Kwa sababu Munguanayejua maneno yote anajua ya kwamba anaweza kufanyakazi hata kubwa kupita kwa njia ya rafiki yako pale kitandani,hivi anamwacha pale.

~ 21 ~Mara nyingine Mungu anafanya neno

ninaloomba kwake hata kama si mapenzi yake?

Ndiyo, anafanya hivi mara nyingine. Labda atafanya hivikama ukimwambia ya kwamba ni lazima kwake kufanya nenounaloomba. Waza juu ya maneno mawili yaliyotokea kwawakati wa Agano la Kale:

1. Bwana alikulisha Waisraeli na mana toka mbinguniwakati waliposafiri jangwani kwendea inchi ya Kanana.Waisraeli walianza kuchoka kula mana hii nyuma ya siku nyi-ngi kidogo, hivi waliomba Mungu na nguvu kuwapa nyamabila kutafuta kufahamu kwanza kama neno hili ni mapenziyake. Mungu aliwapa nyama kama walivyoomba lakini alitumaugonjwa mbaya sana katikati yao vilevile. Soma Zaburi 106:13-15 na Hesabu 11:4-9, 31-33. Unafikili ilikuwa vizuri kwaWaisraeli kuomba Mungu na nguvu kuwapa chakula kingine?

23

OMBA KWA JINA LANGU

Page 24: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

2. Mfalme Hezekia alikuwa mgonjwa sana na Bwana alitu-ma nabii karibu naye kumwagiza kutengeneza maneno yakenyumbani kwa sababu kufa kwake kulikuwa karibu.Inaonekana wazi kwamba yalikuwa mapenzi ya Mungu kwamfalme kufa kwa wakati ule. Lakini Hezekia hakukubali nenohili na aliomba Mungu sana sana aweze kumponyesha. Mungualijibu maombi yake na alimwacha kuishi kwa miaka 15mingine (2 Wafalme 20:1-6). Katika muda huu mwana wakeManase alizaliwa naye aligeuka mfalme wa Yuda nyuma yakufa kwa baba yake. Hezekia alikuwa mfalme mzuri aliye-ongoza watu wake kufuata Bwana lakini Manase alikuwammoja wa wafalme waovu zaidi wa Yuda, akaondosha watuwake karibu na Mungu na kuwafundisha kuabudu sanamu (2 Wafalme 21:1-3,16). Unafikili ilikuwa vizuri kwa Hezekiakuomba Mungu sana sana kumponyesha? Manase asingalizali-wa kama Hezekia angalikufa wakati Mungu alipokusudikwaye kufa.

Mifano hii miwili inatufundisha ya kwamba haifai kwetukuomba maneno na nguvu karibu na Mungu. Sharti tuombeayafanye kama ni mapenzi yake tu. Umwambie Mungumaneno unayotaka ayafanye, lakini acha Mungu kuchaguakama atayafanya au sivyo.

~ 22 ~

INANIPASA KWENDA PAHALIFULANI KWA MAOMBI?

Hakuna agizo ndani ya Agano Jipya kusema sharti tuombekwa pahali fulani tu, na tunaona ndani ya Biblia watu waki-omba kwa pahali mbalimbali:

Elia aliomba Mungu juu ya mlima Karmeli (1 Wafalme18:36).

Hezekia aliomba Mungu kitandani (2 Wafalme 20:2).Saulo aliomba Mungu wakati alipokuwa njiani kwenda Da-

masiki (Matendo 9:6).

24

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 25: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

Petro aliomba kwa dari ya nyumba pahali alipopanga(Matendo 10:9).

Paulo na Sila waliomba gerezani (Matendo 16:25).Hata wewe ni pahali gani, ukifanya neno gani, unaweza na

ingekupasa kuomba Bwana.Ndani ya Waebrania 10:25 tunaagizwa vilevile kukusanyika

na Wakristo wengine kuonyana na kusukumana katika mape-ndo. Bila shaka Wakristo waliomba pamoja kwa wakati ulevilevile. Kwa kufanya hivi tunaweza kukutana ndani ya nyu-mba ya Mungu au ndani ya nyumba ya ndugu Mkristo fulani,au pahali po pote pengine.

~ 23 ~INANIPASA KUSHINDA SAA

NGAPI KWA MAOMBI?Hakuna jibu wazi ndani ya Maandiko Matakatifu kwa ulizo

hili vilevile. Ni desturi nzuri sana, ndiyo desturi ya lazima kwaMkristo kuweka saa fulani kila siku kwa kuomba Mungu pekeyake. Ingempasa kusoma Neno la Mungu kwa wakati huuvilevile na kuacha Bwana kusemana naye kwa njia ya Nenolake. Saa nzuri zaidi kwa maneno haya ni asubui, mbele yakuanza kazi ya nyumba (Zaburi 5:3). Saa hii Mkristo anapati-shwa nguvu rohoni kushinda katika mambo na majaribu yoteyatakayofika kwake kwa mchana ule.

Mara nyingine Mkristo atapenda kushinda saa tatu, ine auzaidi au hata mchana au usiku mzima katika maombi juu yaneno kubwa fulani. Kwa mfano labda unaomba Mungu kuku-julisha nini anataka ufanye, au labda kuna matata fulani ndaniya kazi ya Bwana au maneno mengine yaliyo mazito rohonimwako. Samweli aliomba Mungu usiku mzima (1 Samweli 15:11).Watumishi wengine wa Mungu wanashinda saa mbili au zaidikwa maombi kila siku.

Mara nyingine tunaweza kuomba ombi fupi tu kwa sababusaa inakosa kwa ombi refu. Unakumbuka habari za Nehemia

25

OMBA KWA JINA LANGU

Page 26: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

wakati aliposimama mbele ya mfalme (Nehemia 2:1-8)? llikuwakazi ya Nehemia kuangalia vinyweo vya mfalme na ilikuwalazima kwake kuonekana na furaha kila mara alipotokea mbeleya mfalme. Lakini siku ile alikuwa na huzuni kwa sababualikuwa amepokea habari za huzuni toka Yerusalema. Mfalmealiona huzuni yake, akamwuliza kwa sababu gani hakuwa nafuraha. Halafu Nehemia aliomba Mungu mbio rohoni mwake,labda kwa nusu ya dakika tu angali alikuwa akisimama mbeleya mfalme (sh.4). Bila shaka aliomba Mungu kumpa akili awezekujibu mfalme vizuri. Kisha aliomba mfalme kumruhusu kuru-di kwa inchi ya Yuda kusudi ajengishe tena ukuta wa Yeru-salema, na mfalme alikubali.

Neno kubwa si kama tukishinda dakika ngapi au saa ngapikwa maombi, lakini ni kwa roho zetu kushinda na hali yamaombi wakati wote. Kama ni hivi, itageuka desturi kwasikuomba Mungu mara nyingi kwa mchana mmoja hata wakatitunapofanya maneno mengine. Kwa njia hii tutakuwa naupatano wa karibu, ushirika mtamu sana na Bwana wetuwakati wote.

~ 24 ~INANIPASA KUKAA NAMNA GANI

SAA NINAPOOMBA?Hakuna agizo ndani ya Biblia kusema sharti tusimame au

kuketi au kupiga magoti au kukaa namna yo yote wakatitunapoomba.

Kwa wakati wa Agano la Kale wengine walilala kifudifudiudongoni wakati walipoomba, kama Musa na Haruni (Hesabu16:22), na Yosua (Yosua 5:14). Elia aliinama na kuweka usowake katikati ya magoti yake (1 Wafalme 18:42). Watu wenginewaliinamisha vichwa vyao kama mtumishi wa Abrahamualivyofanya (Mwanzo 24:26); na Waisraeli (Kutoka 4:31; 12:27);na Musa (Kutoka 34:8). Wengine walipiga magoti, kamaSolomono (1 Wafalme 8:54; 2 Mambo 6:13), na Ezra (Ezra 9:5),na Danieli (Danieli 6:10).

26

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 27: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 25 ~

Ni kama watu walisimama kwa maombi wakati BwanaYesu alipokuwa duniani (ona Marko 11:25). Mfarisayo namtoza kodi walisimama wakati walipoomba (Luka 18:10-13).Stefano alipiga magoti wakati alipoomba Mungu kusameheWayuda waliokuwa wakimwua kwa njia ya kumtupia mawe(Matendo 7:60). Petro alipiga magoti wakati alipoomba Mungukufufua Dorika (Matendo 9:40). Paulo alipiga magoti wakatialipoomba pamoja na wazee wa Efeso (Matendo 20:36).

Kwa wakati wa sasa zaidi ya watu wana desturi ya kupigamagoti wakati wanapoomba Mungu peke yao. Wenginewanafanya vivyo hivyo wakati wanapokutana na watuwengine kwa maombi. Ndani ya makusanyiko mengi ya ma-ombi mtu mmoja anasimama na kuongoza wengine kwamaombi nao wanasimama au kuketi wakiinamisha vichwavyao. Watu wengi wanafunga macho yao wakati wanapoombaili maneno ambayo yanawazunguka yasiondoshe mawazo yaokwa maombi.

Hivi tunaona ya kwamba wengine wa watu ambao tunaso-ma habari zao ndani ya Biblia waliomba wakisimama, wenginewalipiga magoti, wengine walilala kifudifudi udongoni. Nenokubwa si kama tukisimama au kupiga magoti au kulala kifudi-fudi saa tunapoomba, lakini kama tukiwa na roho ya kunye-nyekea mbele ya Mungu. Ingetupasa kuomba na roho yaunyenyekevu, tukikumbuka ya kwamba Mungu hana denikwetu. Hatustahili kupokea hata moja ya baraka zake zote;tunaweza kumkaribia kwa njia ya maombi kwa sababu yaneema yake tu.

Kwa wakati wa kuja viumbe vyote mbinguni, duniani, nachini ya dunia watapiga magoti mbele ya Kristo na kutangazawazi ya kwamba yeye ndiye Bwana, kwa utukufu wa MunguBaba (Wafilipi 2:10-11).

27

OMBA KWA JINA LANGU

Page 28: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

~ 26 ~

Ni vizuri kwa mimi kuomba wakati mimi ni pekeyangu tu, au pamoja na watu wengine vilevile?Umejifunza mbele ya kwamba ni sharti kwa Mkristo ku-

omba peke yake kila siku. Ona ukurasa 25 na kuusoma tena.Ulisoma vilevile ya kwamba tunapaswa kukusanyika pamo-

ja na Wakristo wengine kwa kusukumana katika mapendo nakazi nzuri (Waebrania 10:24-25). Tunafanya hivi kwa njia yakusoma Neno la Mungu na kuomba na kusifu Mungu pamoja(Waefeso 5:19-20; Wakolosayi 3:16). Mungu ametupa sisi agizohili kwa sababu anajua ushirika pamoja na Wakristo wengineutatusaidia. Bila maneno haya roho zetu zinapoa mbio mbio.

Waamini walianza kukutana pamoja kwa maombi maramoja nyuma ya kurudi kwa Bwana Yesu Kristo mbinguni(Matendo 1:14). Kisha karibu watu 3000 waliamini siku yaPentekote. Watu hawa walikutana pamoja kwa maombi (Ma-tendo 2:41-42). Katika Matendo 12:5,12 tunaona ya kwambaWakristo wengi walikuwa wamekutana nyumbani mwa Mariakuombea Petro aliyekuwa gerezani kwa wakati ule. Naye ali-funguliwa.

Kuna ahadi nzuri sana kwa hata watu wawili wanaopatanakuomba juu ya neno fulani. Yesu alisema neno hili litafanywana Baba yake mbinguni (Matayo 18:19)!

~ 27 ~INAPASA MTU KUOMBA NAMNA GANI

KATIKA KUSANYIKO LA WAKRISTO?Katika makusanyiko ya Wakristo mtu mmoja anasimama

kuongoza watu wote walio pale kwa maombi. Wakati anapo-maliza, mtu mwingine anasimama na kufanya vivyo. Ingepasawatu hawa kusema na sauti ya nguvu kidogo ili watu wote

28

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 29: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

waweze kuwasikia. Vizuri waombe kwa mambo yale yaliyomzigo wa Wakristo wote pale, si kwa mahitaji yao wenyewe.

Sharti wale wanaoongoza watu wengine kwa maombi wa-taje maneno fulani mbele ya Mungu. Haifai waombe, “Bwana,bariki watumishi wako wote pahali pote duniani,” lakini“Bwana, bariki ndugu zetu fulani waliokwenda kuhubiriHabari Njema yako kwa kijiji fulani.” Sharti wamwambieMungu nini wanayotaka afanye kwa ndugu hawa, wakitajanamna ya kazi yao na mahitaji na masumbuko yao yote mbeleyake. Mungu anataka sisi kumwambia wazi nini tunayotakaatufanyie kama ikipatana na mapenzi yake. Halafu wakatiBwana anapojibu maombi yetu tunafahamu kwamba anajibumaombi fulani. Neno hili litatusukuma kumsifu na kumshuku-ru, na litatupa hamu kudumu katika maombi.

Kuna maneno mawili ambayo inakupasa kuepuka wakatiunapoongoza watu wengine katika maombi:1. Usiongoze watu kwa maombi kusudi uonekane kama

Mkristo mzuri mbele yao! Ona Matayo 6:5.2. Usiombe maombi marefu marefu ya masemo mengi. Bila

shaka wengine ndani ya kusanyiko lenu la maombi wanamzigo rohoni vilevile juu ya maneno mengine wanayotakakuyaleta mbele ya Bwana. Kwa sababu hii si vizuri kwa mtummoja au watu wawili kumaliza saa nzima iliyowekwa kwamaombi.

~ 28 ~

MAOMBI YATAGEUZA MAISHA YANGU KWA NJIA YO YOTE?

Ndiyo. Waza juu ya maneno haya matatu:1. Maombi yatakupa FURAHA. Bwana Yesu alisema,

“Mwombe, na mutapata, furaha yenu itimizwe” (Yoane 16:24).Utafurahi sana kuona Bwana akifanya maneno yale ambayo

29

OMBA KWA JINA LANGU

Page 30: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

ulimwomba kufanya kwa sababu utafahamu ya kwamba yeyeni karibu sana nawe na anakufikili pamoja na maneno yakoyote. Ni kusema wewe na Bwana wako muna upatano mtamusana.

2. Utapata NGUVU mpya kwa njia ya kungojea Bwana kwamaombi (Isaya 40:31), ndiyo nguvu ya roho kushinda majaribuna kudumu katika kazi ya Bwana hata wakati wa matata namazuizo. Mara nyingine Bwana ataongeza hata nguvu yako yamwili kama ukihitaji nguvu kubwa kupita kumtukuza yeye.

3. SALAMA ya Mungu itajaza roho yako kama unawekamahitaji na mafazaiko yote mikononi mwa Bwana kwa sababuunajua Bwana Yesu ataangalia maneno haya yote na kute-ngeneza yote kwa baraka yako. Soma Wafilipi 4:6-7.

~ 29 ~

MAOMBI YANA FAIDA GANIKWA KAZI YA BWANA?

Maombi ya watu wa Mungu yanafanya kazi nyingikusaidia Habari Njema kuendelea mbele kwa sababu kunauwezo na baraka ndani ya maombi (Yakobo 5:16). Tunawezakuona neno hili katika maisha ya Elia wakati Bwana alipojibumaombi yake na kufufua kijana aliyekufa (1 Wafalme 17:21-22).Mbele ya wakati ule Elia aliomba Mungu kuzuiza mvuaisinyeshe. Alitaka kuonyeshea watu wa Yuda ya kwambaMungu aliwakasirikia kwa sababu ya zambi zao. Bwana alijibumaombi ya Elia na mvua haikunyesha kwa miaka mitatu nanusu (Yakobo 5:17). Halafu wakati watu waliporudi karibu naMungu Elia aliomba Mungu kutuma mvua tena na mvua ili-anza kunyesha (1 Wafalme 18:41-46).

Wakristo kwa wakati wa mwanzo wa Kanisa waliombaBwana kuwapa uhodari kumshuhudia wakati adui zao walipo-

30

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

Page 31: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

jaribu sana kuwaogopesha. Mungu alijibu maombi yao? OnaMatendo 4:29-31.

Hakuna neno Mungu asiloweza kufanya kwa kujibumaombi ya wale wanaokaa ndani ya Kristo (Yoane 15:7). Watuhawa wanaomba tu kwa maneno yale yanayopatana na mape-nzi ya Mungu kwa sababu mawazo yao yanaongozwa na Nenolake, hivi Mungu anaweza kufanya maneno wanayoombakwake.

Unataka Mungu kufanya nini ndani ya maisha yakomwenyewe na kazi yako kwaye? Unataka afanye nini ndani yamaisha na kazi ya watu wengine? Kuna pahali pengine dunianiHabari Njema isipoweza kuingia nawe ungependa sana watuwa pahali pale waweze kuisikia vilevile? Kuna watu wengineambao uliwafudisha juu ya njia ya wokovu tena na tena lakinimioyo yao ni migumu kama mawe? Mungu atafanya manenoyasiyowezekana kwa watu kwa sababu ya maombi yako kwanikuna uwezo kwa maombi. Tumika na uwezo huu kwa utukufuwake na utabarikiwa zaidi.

~ 30 ~

NAMNA GANI NINAWEZAKUJIFUNZA KUOMBA?

Unauliza vizuri. Wanafunzi waliomba Bwana Yesu kuwa-fundisha kuomba. Alifanya hivi kwa njia ya kuwapa mfano wamaombi tuliosoma katika Luka 11:1-4. Tuliwaza juu ya mfanohuu mbele.

Halafu fikili juu ya mtoto na baba yake. Inapasa mtoto kuji-funza namna gani kuomba baba yake kwa kitu fulani? Sivyo,hahitaji mtu kumfundisha namna gani kuomba kupewa kituanachotaka. Anasema tu, “Baba, tafazali unipe maji nipate ku-nywa.”

31

OMBA KWA JINA LANGU

Page 32: OMBA KWA JINA LANGU - Everyday · KWA JINA LANGU” “Na mukiomba lo lote kwa jina langu, nitalifanya, Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Kama mukiomba neno gani kwa jina langu nitalifanya.”[Yoane

Halafu kumbuka ya kwamba Mungu ni Baba yako ya mbi-nguni. Unahitaji kweli kujifunza namna gani kuomba Babayako ya mbinguni kwa mahitaji yako? Labda hujui kusemamaombi yako na maneno marefu mazuri mazuri, lakini nenohili si kitu kwa Mungu. Anakusikia hata hujui kusema vizurikwa sababu wewe ni mtoto wake naye anakupenda. Anajuaroho yako yote.

Kuna maneno mengi tunayojifunza kwa njia ya kujaribukuyafanya, kama kutembea, kusema, kusoma, na mengine. Nivivyo hivyo na maombi. Kwa kipimo unachoomba, kwa kipimohiki utajua namna gani kuomba. Mungu atupe sisi sote hamukubwa kugeuka mafundi kwa maombi!

32

MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI