mtakuja development project - ft kilimanjaroft kilimanjaro · rasimu ya katiba - rasimu ya katiba...

11
Mtakuja Development Project 2011 1 | Page Mtakuja Development Project Shughuli za mwaka wa tatu Juni 2010 hadi Mei 2011 Mtakuja Village Kilimanjaro Region Tanzania The Mtakuja Development Project is an initiative supported by FD Kilimanjaro, an international NGO registered in the Netherlands and Tanzania.

Upload: others

Post on 24-Oct-2019

36 views

Category:

Documents


1 download

TRANSCRIPT

Page 1: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

1 | P a g e

Mtakuja Development Project

Shughuli za mwaka wa tatu – Juni 2010 hadi Mei 2011

Mtakuja Village – Kilimanjaro Region – Tanzania

The Mtakuja Development Project is an initiative supported by FD Kilimanjaro, an international NGO registered in the Netherlands and Tanzania.

Page 2: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

2 | P a g e

MAENDELEO ENDELEVU NA USHIRIKI WA JAMII

Chama cha Maendeleo ya Jamii Mtakuja kimekuwa na tabia ya kuwa na mikutano ya kila mwezi.

Kuunda umiliki wa ndani - Bodi ya vikao vya chama imepokea mafunzo 8 kutoka Floresta juu ya masomo kama uongozi na ujenzi wa taasisi.

Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa.

VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa mapema mwaka 2009.Wakati wa

mwaka wa tatu wa mradi huo, vikundi viliendelea kukuza akiba zao na kupokea mafunzo.

Kukopa kunakadiriwa kufanyika ni kati ya Tshs. 7 m. Jumla ya akiba kwa ajili ya makundi yote ni

mpaka kufikia Tsh. 11 m (au € 5000).

SACCOS – Ofisi ya SACCOS ( Chama cha Ushirika cha kuweka na kukopa) ilifunguliwa katika kijiji

cha Mtakuja. Uanzishwaji wa SACCOS unapaswa kuongeza upatikanaji wa huduma za kuweka

akiba kitaaluma zaidi na huduma za mikopo. Wakulima katika mpango wetu wa umwagiliaji

wana fursa ya kupatiwa mikopo.

MAPATO & KILIMO Uanzishwaji wa chama cha uwezo wa ndani. Kamati ya wanachama 15 iliundwa ikiwa na

wawakilishi wa kijiji. Baada ya muda fulani, kamati itachukua jukumu la usimamizi wa jumla na

usimamizi wa mradi na hasa mpango wa umwagiliaji.

Uzalishaji mazao. Wakulima 95 walichaguliwa na kulima nusu ekari katika mashamba ya mfano.

Waliamua kuanza na mahindi na mavuno yanatarajiwa mwezi Septemba. Wanawake ni 60% ya

wakulima waliochaguliwa.

Wakulima viongozi - wakulima viongozi 8

na wakulima viongozi wasaidizi 8 walipewa

mafunzo na kuanza kazi yao kwa kujitolea.

Mkulima kiongozi na msaidizi kwa pamoja

huongoza vishamba vya umwagiliaji yenye

wakulima 24 katika mashamba ya mfano.

Wao hupata mafunzo ya kila mara na

hufanya kazi kwa bidii sana.

Mseto wa mazao ya biashara - Majaribio

kwa mazao mengine yenye faida

yameanzishwa.

Page 3: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

3 | P a g e

AFYA Kambi ya matibabu kwa watoto - Kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Uholanzi

uchunguzi wa matibabu kwa watoto (MCC) na katika ushirikiano wa karibu na hospitali ya TPC

na kituo cha afya cha kijiji walikuwa wenyeji wa kambi ya pili ya kila mwaka ya matibabu.

Watoto 1,226 wenye umri chini ya miaka 10 walifanyiwa tathmini, kutibiwa na inapokuwa

muhimu walihamishiwa kwa watoa huduma za afya wa kawaida na timu ya wataalamu wa afya

11 kutoka MCC. Mwaka huu wataalamu kwa ajili ya ulemavu, macho na meno walijiunga na

kambi.

Huduma ya mtu binafsi - Watoto wenye haja ya huduma ya matibabu ya haraka wamekuwa

wakisaidiwa na FDK kwa upasuaji kuanzia kukarabati ‘cleft palate’, upasuaji wa shida ya njia ya

mkojo na upasuaji wa mguu iliyopinda ‘club foot’. Upasuaji wote ulikuwa ukifanyika hapa

Tanzania.

Kusaidia watoto wenye ulemavu – FDK wanashirikiana na shirika lisilo la kiserikali CCBRT

(Comprehensive Community Based Rehablitation in Tanzania) kutoa miundo ya ukarabati

waviungo kwa watoto wenye ulemavu katika kijiji cha Mtakuja. Hesabu ilitolewa ya watoto

wenye ulemavu na wao kusaidiwa kutokana na ushirikiano huo.

Kituo cha elimu ya kuzuia magonjwa – Kwa

msaada kutoka Rotary Club (Soet-

Baarm/Ahlen) kituo cha elimu ya kuzuia

magonjwa kilijengwa. Hiki ni kituo cha afya

vijijini cha mkazo maalum juu ya kuzuia

maambukizi kwa njia ya mafunzo,

maonesho na kuwezesha upatikanaji wa

habari. Pia huduma za afya ya msingi

itatolewa. Timu ya wafanyakazi wa afya ya

jamii imepatiwa mafunzo ya kutumikia

jamii.

ELIMU Chakula cha mchana shuleni - Kwenye shule mbili za msingi na shule tatu za awali vyakula vya

mchana 180,310 vilitolewa kwa wanafunzi 968.

Taa za nishati ya jua – Taa 500 zinazotumia nishati ya jua zimegawanywa kwa wanafunzi wa

shule ya msingi. Kwa njia hiyo wakati wa giza wanaweza kufanya kazi zao za nyumbani

wanazopewa kutoka shule na kuboresha matokeo yao.

Masaa ya ziada ya mafundisho – Walimu katika shule za msingi wamefundisha masaa 8,188 ya

ziada baada ya masaa ya kawaida ya shule na hapo hupokea motisha kidogo kila mwezi kutoka

FDK.

Page 4: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

4 | P a g e

Shule ya awali na uwanja wa michezo – Shule ya msingi ya awali iliyo katika kitongiji cha

Wamasi cha jirani – Remiti- Mtakuja kimemalizika na kufunguliwa rasmi. Kando yake uwanja

wa michezo ulianzishwa. Kina sifa mbalimbali na

madhumuni ya kuwawezesha watoto wadogo kukuza

vipaji.

Mipango ya udhamini - Programu ya mwaka ya

udhamini wa wanaohitimu shule ya msingi iliendelea

kwa wanafunzi 10 wengine wenye kufanya vizuri

kupelekwa kwenye shule binafsi ya sekondari iliyopo

Mtakuja.

Msaada katika shule za sekondari - Ilitoa bajeti kusaidia

shule ya sekondari Mtakuja katika ujenzi wa madarasa

ya ziada ili kutosheleza ukuaji mkubwa wa idadi ya

wanafunzi katika shule.

Mafunzo ya ufundi stadi - Mpango wa udhamini kwa

ajili ya mafunzo ya ufundi umeshaanza. Wanafunzi 6

waliochaguliwa wanajifunza ujuzi wa vitendo.

MIUNDOMBINU Barabara - TPC Ltd imesaidia kujenga karibu km 4 za barabara kuwezesha kufika katika shamba

la mfano, ikiwa ni pamoja na barabara ndogo ndani ya shamba.

Umeme – Ujenzi wa usambazaji wa nishati, km 4 za miundombinu umeme, ikiwa ni pamoja na

transformer, ilifanywa na kampuni ya usambazaji wa umeme Taifa, ilikamilika Januari 2011.

Uunganishaji na maandishi yote yalikamilika mwezi Machi.

Mpango wa umwagiliaji – nusu ya eneo la mpango wa umwagiliaji, hektari 20 umemalizika.

Mpango huu hutumia mfumo wa bomba msukumo, ambapo mabomba makuu na matawi yake

yamefukiwa ardhani. Ilikuwa ni kazi kubwa yenye vikwazo vingi lakini ilimalizika baada ya kupata

umeme. Hivi sasa utaratibu wa vinyuyizii unatumika kumwagilia vishamba 96 ya nusu eka kila

kimoja.

Maji – Mnamo Julai 2009 visima viwili

vilichimbwa na vinafanya kazi sasa. Maji

yanatumika kwa ajili ya umwagiliaji lakini

pia vituo vya maji ya matumizi ya

nyumbani vimeanzishwa.

Ofisi ya shamba – ofisi ilijengwa katika

eneo la shamba la mfano na kutumika

kama eneo la vikao na kuhifadhia vifaa. Ni

yenye muundo wa veranda kubwa yenye

kukidhi aina mbalimbali za mikutano na

vikao vya kijiji.

Page 5: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

5 | P a g e

WAFANYAKAZI Watumishi - FD Kilimanjaro ina wafanyakazi wawili ambapo wameajiriwa kwa muda mrefu. Zablon

Sarakikya ni afisa programu ya kilimo anashughulika na shamba la mfano lakini pia ana jukumu

muhimu kuwasiliana na uongozi wa kijiji. Stela Msarikie kutoka Mtakuja ni afisa ustawi wa jamii na

ana jukumu muhimu la kudumisha mawasiliano na kushirikisha wanajamii, hasa wanaoishi katika

mazingira magumu. Kijiji kimeajiri walinzi watatu na msadizi wa umwagiliaji kwa ajili ya shamba la

majaribio.

Mwaka wa tatu – kuendelea kuweka mpango katika vitendo

Kama inavyoonekana hapo juu, katika mwaka wa tatu Mradi wa Maendeleo Mtakuja

umeshatekeleza shughuli nyinngi, kupitia katika maeneo yetu makuu ya programu afya, elimu, kilimo

na mapato na miundombinu.

Tunatafuta kushirikisha jamii wakati wote,

kuanzia kufanya maamuzi mpaka mipango ya

fedha na michango yote. Mikutano inaandaliwa

katika ngazi za vitongoji na mikutano na

viongozi wa kijiji hufanyika mara kwa mara na

mara nyingi huwa sio rasmi.Imekuwa wazi

kwamba wigo wa mradi na fursa zake ni vigumu

kueleweka kwa wanajamii wengi, lakini uelewa

wao ni muhimu kwa mafanikio ya mradi ya

muda mrefu. Kama mmoja wa washirika wetu

wa Tanzania anasema:”Mbali na mambo

mengine umasikini unaathiri mawazo ya watu

na tabia”.

Katika miaka ijayo, usimamizi wa majukumu ya

mradi yatatakiwa kuchukuliwa na wanajamii.Kuunda chombo kwa ajili ya hili, kamati ya mradi

iliundwa ikiwa na wanachama 15, ambao wanatakiwa kupitishwa katika chama na kuwezeshwa na

halmashauri ya kijiji. Hii inathibitisha kuwa ni njia yenye ugumu lakini yatupasa kuifuata.

Hatua kubwa ilikuwa mwanzo wa kilimo katika mashamba ya majaribio. Sasa hectari 20 za mwanzo

zinalimwa na wakulima 96 waliochaguliwa na wanajamii. Ujenzi wa miundombinu ya usambazaji wa

nishati ya umeme ulianza Aprili 2010 na ulichukua muda mrefu kuliko ilivyotegemewa mpaka kupata

umeme wa uhakika Januari 2011. Shamba la mfano ni kitovu cha mradi huu, mpango wa kuongeza

hectari 20 nyingine tayari upo katika matayarisho. Matokeo yanayotegemewa kama pato la kilimo

Kulinda uendelevu na matokeo ya kudumu ya utekelezaji wa kazi za mradi hata baadaya kipindi

cha muda wa mradi.

Kuongeza mapato ya mwaka ya wanajamii kupitia kuongeza mapato kutokana na kilimo na

shughuli nyingine za kibiashara, wakati huo tunahakikisha kila mtu katika jamii anapata milo

mitatu kwa siku kwa mwaka mzima.

Page 6: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

6 | P a g e

katika shamba lililomwagiliwa inatakiwa kuthibitisha ongezeko kubwa la usalama wa chakula wa

watu kwa muda ikiwepo na kuongeza ardhi ya kumwagiliwa – kuongeza pato la kilimo itapelekea

ongezeko la ngazi za pato la ziada. Kilimo ni mpango w amuda mrefu haitasababisha mfululizo wa

ukuaji kiuchumi, bali kitaboresha usalama wa watu katika chakula, kinga dhidi ya majanga ya

kiuchumi,kuboresha hali za kiafya na kutoa msingi kwa ajili ya watu kuendeleza vyanzo vingine vya

mapato na shughuli nyingine za kiuchumi.

Mashamba ya majaribio inaonekana kuwa na

mazao ya mahindi yenye afya wakati mazao ya

katika maeneo mengine ya kijiji yalishindwa kwa

sababu ya ukame. Ilihitaji juhudi kubwa kufikia

hapa, wanajamii walifanya kazi kwa pamoja ili

kusafisha eneo la majaribio, kuondoa vichaka,

miti na visiki vya miti na kuchimba mitaro kwa

ajili ya mabomba na kuondoa visiki 100 vya miti

mikubwa.

Wakulima viogozi wa Mradi na wasaidizi wa

wakulima viongozi ni mfano wa wanakijiji wenzao na kucheza nafasi ya kijamii katika jamii. Wapo 16

wanaume na wanawake waliochaguliwa kutoka kwa wanajamii ili kuongoza wakulima katika juhudi

zao za kilimo.

Shamba la majaribio kwa sasa hutumiwa na wakulima 96 na mara baada ya kukamilika, ekari 100 ya

ardhi iliyomwagiliwa itawezesha karibu wakulima 190 (ikiwa ni pamoja na wakulima viogozi) kwa ajili

ya kulima nusu eka kwa msimu. Wakulima wa kwanza walichaguliwa na viongozi wa vitongoji kwa

kuangalia jitihada zao za kufanya kazi ya jamuiya na katika kuandaa shamba. Kupitia mfululizo wa

mikutano ya hadhara katika ya vitongoji. Majina ya wakulima waliochaguliwa yaliwekwa wazi kwa

umma. Wakulima wengi ni wanawake na vitongoji kuwakilishwa kufuatana na idadi yao ya wakazi.

Mwaka wa 3 umeona hatua muhimu katika kufikia malengo ya programu ya afya. Kwa msaada

kutoka kwa klabu ya Rotary ya Soet-Baarm (Uholanzi) na Ahlen (Ujerumani) mradi umejenga kituo

cha afya kwa lengo maalum juu ya kinga na kuanzisha timu ya wafanyakazi wa afya ya jamii.

Wafanyakazi wa afya ya jamii wana kawaida ya kutoa mafunzo ya msingi – kwa kuzunguka au

majumbani - huduma za afya, lakini pia kutafuta na kuhamasisha na kuongoza vizuri wagonjwa na

familia ili kupata huduma zetu za afya.

Kwa sababu kuna zahanati na hospitali karibu si vizuri sana kujenga zahanati au kliniki nyingine.

Matatizo ya afya kwa Mtakuja yanaonesha kuwa kuna masuala mengi ya afya kuhusiana na hali duni

ya maisha, usafi wa mazingira, ukosefu wa elimu, usafi, dawa za kuzuia na chanjo; kwa ufupi kinga.

Kwa sababu hizi inaonekana bora zaidi kuwa na lengo la kuzuia na huduma za afya ya msingi. Kituo

cha kuzuia kitakuwa kuzingatia wenyeji wote wa Mtakuja (4500) kwa kuzuia na upande wa Kusini wa

kijiji kwa ajili ya huduma za afya ya msingi (ina karibu watu 2200).

Kuongeza upatikanaji na utumiaji wa huduma za afya ya msingi ndani ya nchi na ziada ya huduma

maalumu zaidi, wakati huo kuboresha afya kwa ujumla na uelewa wa masuala ya afya na

magonjwa.

Page 7: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

7 | P a g e

Wafanyakazi wa afya ya jamii wamechaguliwa

kutoka kijijini na kupata mafunzo kutoka

Hospitali ya TPC na Wizara ya Afya. Ni

wanawake 3 na wanaume 2 na kwa sasa

wanafanya kazi kikamilifu katika kijiji kuelimisha

watu katika usafi wa mazingira, afya na huduma

ya afya ya msingi. Pamoja na kituo, nyumba za

wafanyakazi zimejengwa kwa ajili ya malazi ya

baadhi ya wafanyakazi wa afya ya jamii ya

utunzaji wa kituo na inapopatikana kwa

dharura.

Kazi ya kituo cha kuzuia magonjwa na wafanyakazi wa afya ya jamii ni:

Kupima uzito wa watoto,

Ushauri wa lishe,

Huduma za kabla na baada ya kujifungua,

Huduma ya kupima upungufu wa damu na usambazaji wa kuongeza madini ya chuma,

Kampeni ya vitamini A,

Kampeni dhidi ya minyoo,

Chanjo,

Elimu ya akina mama,

Elimu katika usafi na usafi wa mazingira.

Kambi ya Kituo cha matibabu, mara moja kwa mwezi kwa ajili ya walemavu, mara moja kwa

mwezi kwa ajili ya huduma za meno, mara mbili kwa mwaka kwa matatizo ya jicho na mara

mbili kwa mwaka kwa ajili ya matatizo ya Masikio Pua na Koo.

Upimwaji wa VVU / UKIMWI na ushauri mara moja kwa mwezi,

Rufaa ya matatizo ya afya kwenda hospitali ya TPC au kwa mtaalamu.,

Huduma ya kufuatiliwa baada ya

wagonjwa kurudi nyumbani,

Muendelezo wa maonyesho ya taarifa za

matibabu,

Kituo kwa ajili ya wafanyakazi wa afya ya

jamii,

Kushirikiana na taasisi na mashirika husika.

Mnamo Agosti 2010 tukiwa pamoja na shirika

lisilo la kiserikali Kontrollerna Matibabu kwa

Watoto (MCC) kwa ajili ya shirika la wataalamu

wa kujitolea katika huduma za afya tulipanga

kambi ya pili ya matibabu. Timu ya watu 11 ya kujitolea wenye historia mbalimbali za afya, walikuja

Mtakuja kufanya tathmini ya afya ya msingi ya watoto na kutoa huduma ya juu kwa ajili ya safu ya

tathmini ya matibabu na huduma za afya.Tathmini ililenga sana juu ya utapiamlo masuala mengi

yanayohusiana na afya, ikiwa ni pamoja na minyoo , upungufu wa damu, upungufu wa vitamini na

matatizo ya ngozi na mambo mengine.

Page 8: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

8 | P a g e

FD Kilimanjaro iliwashirikisha hospitali ya TPC katika kutoa huduma ya awali za kufuatilia, ikiwa ni

pamoja na maabara ya uchambuzi wa sampuli za kinyesi, mkojo na damu. Kwa kuwashirikisha TPC

hospitali ni uhakika kwetu sisi kwamba watoto wowote waliokutwa na matatizo ya afya, ambayo

inahitajika kufuatilia au huduma ya kuendelea

watapata huduma bora inayohitajika. Katika

mtukio mengi FD Kilimanjaro waligharamia

gharam zote za ufuatiliaji. Wakati wa kambi ya

pili ya matibabu timu ya MCC iliwahudumia

watoto 1223. Wafanyakazi wa MCC walifanya

kazi pamoja na timu ya wanawake kutoka

ambao walifanya kazi kama watafsiri na

wakalimani.

Wakati wa kambi ya mwaka 2010, TPC hospitali

ilitoa muuguzi mfanyakazi wa VVU / UKIMWI

kwa taarifa na ushauri nasaha kwa familia

zinazopenda kupata elimu na mtaalamu wa meno kwa ajili ya kuangalia meno na kutoa maelekezo

ya namna ya kusafisha meno. Mwaka 2010 pia tulimtambulisha mshirika wetu katika huduma ya

afya Comprehensive Community Based Rehabilitative Care Tanzania (CCBRT) ndani ya kambi. Wao ni

maalum kwa watoto walemavu na walitambua kesi zaidi ya 20 kubwa sisi tulitoa msaada na

ufuatiliaji kwa mwaka mzima. Wengine walifanyiwa upasuaji, wengine kupokea zana maalum na

mazoezi. Kila wiki baadhi ya watoto wenye ulemavu wanatembelewa na kupata huduma.

Elimu inabakia sehemu muhimu ya mradi huu. Katika mwaka wa 3 tuliendelea kupanua mipango ya

chakula cha mchana katika shule za msingi na kupanua wigo shule 3 za chekechea. Tuliendelea na

programu ya masaa ya ziada ya masomo ambapo wanafunzi wa shule za msingi hupata masomo ya

ziada baada ya masaa ya kawaida ya shule na wakati wa likizo. Shughuli hizi bado hazijaonyesha

ongezeko katika matokeo ya elimu.

Wakati wa mwisho wa mwaka 2010 wa shule, asilimia 39% tu ya wanafunzi walifaulu mitihani yao ya

mwisho na kuwawezesha kuendelea shule ya

sekondari. Tunafanya kazi katika hili kwa

kusaidia shule za msingi katika programu ya

kuboresha matokeo kwa kuongeza idadi ya

vitabu kutoka kitabu kimoja kwa wanafunzi

watano hadi kitabu kimoja kwa wanafunzi

wawili. Pia vifaa vya elimu vya ziada

vilinunuliwa kama madaftari, ubao wa rangi,

vitabu vya rejea, rula n.k. Elimu ya msingi

inaathiriwa na sababu nyingi, moja ni kwamba

wazazi hawatambui umuhimu wake.

Kuongeza upatikanaji na matumizi ya elimu bora ya awali, msingi na sekondari na kukuza

machaguo kwa ajili ya elimu ya ufundi na elimu ya watu wazima.

Page 9: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

9 | P a g e

Mwishoni sisi tunatoa msaada kwa mashule katika jitihada zao za kuboresha ufahamu wa kiingereza

kwa mwanafunzi kupitia madarasa ya ziada.

Mwaka 2010 tulikamilisha ujenzi wa chumba cha darasa la shule ya awali ya msingi katika kitongoji

cha Wamasai kiitwacho Remiti. Darasa hilo ni sehemu muhimu ya Shule ya Msingi Mserikia na chini

ya usimamizi wa mwalimu mkuu wa shule hiyo. Watoto wadogo wa Kimasai sasa wanaweza kuanza

shule katika umri wa miaka 4 au 5, Na wakati huo hakuna kukabiliana na mwendo mrefu katika njia

ya vichakaiendayo Shule ya Msingi Mserikia. Kama ilivyo katika mipango yetu jamii imetoa mchango

mkubwa wa fedha na nguvukazi. Wizara ya elimu imeleta mwalimu mpya na jamii imeajiri

mfanyakazi msaidizi wa elimu ambaye anajua lugha ya Kimasai. Sasa darasa lina wanafunzi 42.

Uwanja wa michezo kama shughuli tofauti ulitengenezwa katika shule ya chekechea na watu wa

kujitolea. Kucheza ni muhimu na husaidia sana katika maendeleo ya mtoto na pia wanafurahia.

Mnamo Agosti 2010 mpango wa udhamini wa sekondari uliendelea katika awamu yake ya

pili.Programu ina mpango wa kupeleka wanafunzi wanaofaulu vizuri kutoka kwenye shule mbili za

msingi Mtakuja kwenda kwenye shule ya kibinafsi ya sekondari iliyopo kijijini. Katika wahitimu 10 wa

mwaka jana 8 katika yao wamefaulu vizuri sana na kuendelea na kidato cha II.Wahitimu wengine 10

wamechaguliwa na wameshaanza kidato cha I.

Wanafunzi wamepokea misaada kwa asilimia 70

hadi 100 na wanasaidiwa kwa miaka minne ya

shule ya sekondari,inategemea na matokeo

mazuri ya kila mwisho wa mwaka.

FD Kilimanjaro imeanzisha programu ya

udhamini wa mafunzo ya ufundi stadi kwa

kusaidia wadhaminiwa 6 wa mafunzo ya ufundi

stadi.Uchaguzi wa makini ulifanyika kwa kufuata

hatua ya kuangalia wanajamii wanaopendelea kuomba udhamini waombaji watakaofanikiwa

watafanyiwa usahili. Tulichagua wasichana 4 na wavulana 2 kujiunga na kozi kama: umeme na

mabomba.

FEDHA ZA 2010 FD Kilimanjaro ilikuwa na bajeti ya Euro 370000 kwa mwaka 2010 ambayo ilitumika kama ifuatavyo:

Page 10: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

10 | P a g e

Kuendelea mbele mwaka wa nne

Kwa kuangalia mwaka nne tunategemea mwaka mwingine wa furaha. Mchakato muhimu utafanyika

wa kuanzisha msingi wa uendelevu wa mradi huo na kurasimisha na kuendeleza umiliki wa ndani.

Tutaendelea kusonga mbele na kupanua shamba la mfano na kuwawezesha wakulima. Ushirikiano

na makampuni utaendelea kugunduliwa kwa kupanda maua, mbegu n.k. Mwaka 2011 tutaanza

kutumia kituo cha kuzuia magonjwa na kutarajia mambo mengi kutoka kwa wafanyakazi wa afya ya

jamii ili kupambana na matatizo ya afya ya kawaida kuhusiana na afya na lishe. Kambi nyingine ya

matibabu itapangwa pamoja na MCC. Mwezi Septemba wafanyakazi wa filamu watatengeneza

makala nyingine kama walivyofanya mwaka 2009. Ni tathmini ya kuonekana ya mradi na ni matokeo

ya maisha katika kijiji, lakini pia kutumika kwa ajili ya kubadilishana habari kati ya kijiji na washirika.

Tunaendeleza programu zetu za udhamini ili kuongeza nafasi za ajira. Mradi unahitaji kuangalia kwa

umakini zaidi shughuli za kielimu kuangalia namna gani matokeo ya shule ya msingi yataboreshwa;

kitu kingine tulichopanga ni ujenzi wa nyumba za walimu kuboresha mazingira yao yakuishi. Kwa

kujenga makazi madogo pamoja na kujenga kituo cha kuzuia tunataka kujenga mazingira salama ya

kuishi na pia kufurahia maji katika maeneo ya jirani kwa kufanya hivyo kuvutia walimu. Mwaka 2011

tunategemea kuanzisha ushirika na Heifer International kuleta programu ya mifugo Mtakuja,

programu hii itawezesha familia zenye matatizo zaidi waweze kujipatia vyanzo vya mapato na nafasi

ya kuboresha lishe yao kwa kuanzisha unywaji wa maziwa, mayai au nyama katika mlo wao. Pia

tunaendelea kuwezesha familia kwa kununua taa za ruzuku za nishati ya jua kuleta mwanga usiku

kwenye nyumba zao na kuwezesha watoto wanaokwenda shule kujisomea usiku. Baadhi ya mawazo

mapya yatakuwa yanaendelea kugunduliwa kama vile uhifadhi wa chakula na matumizi ya gesi asilia.

Pamoja na hayo yote, tutaendela kuendeleza programu zetu na kuendelea kujenga ushirikiano

ambao tumeshaujenga hadi sasa, na kuendelea kutafuta ushirikiano mpya wenye faida na mashirika

mengine ya kushirikiana nayo.

Page 11: Mtakuja Development Project - FT KilimanjaroFT Kilimanjaro · Rasimu ya katiba - Rasimu ya katiba ya chama ilitolewa. VICOBA – Vikundi saba vya benki ya vijiji ya jamii viliundwa

Mtakuja Development Project 2011

11 | P a g e

www.fdkilimanjaro.org

Tunawashukuru washirika wetu wote na wanaotusadia:

TPC Ltd. Na Hospitali ya TPC, Kliniki ya Macho KCMC, Floresta Tanzania,Kituo cha Mafunzo ya Kilimo

Kilimanjaro (KATC), AquaTech Ltd, Comprehensive Community Based Rehabilitation in Tanzania

(CCBRT), D-light, FERT & USAWA, Wilaya ya Moshi Vijijini, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro,

Medical Checks for Children (MCC), Mama International, Zero-kap, na Stichting End of Poverty.

Wadhamini wa fedha wa awali na wadhamini waanzilishi wa FD Kilimanjaro ni Stichting FEMI. Mradi

wa Maendeleo Mtakuja umepokea msaada wa ziada kutoka Stichting DIRA 1, The Rotary Club Soest

Baarn ( na washirika wa shirika la Rotary Ahlen, Germany), De Wilde Ganzen, MCC, Rooms

Katholieke Stichting Bijzondere Gezondheidszorg (SBG) na Net4Kids; wote ni wa Uholanzi. Kwa

Tanzania tunashukuru tumepokea msaada kutoka kwa Rural Energy Agency (REA), Programu ya

ushirikishwaji na kuwezeshwa katika maendeleo ya kilimo (PADEP) na Kampuni ya TPC.